Psalms 64:2-6


2 aUnifiche kutokana na shauri la siri la waovu,
kutokana na zile kelele za kundi la watenda mabaya.


3 bWananoa ndimi zao kama panga
na kuelekeza maneno yao kama mishale ya kufisha.

4 cHurusha mishale kutoka kwenye mavizio kwa mtu asiye na hatia,
humrushia ghafula bila woga.


5 dKila mmoja humtia moyo mwenzake
katika mipango mibaya;
huzungumza juu ya kuficha mitego yao,
nao husema, “Ni nani ataiona?”

6 Hufanya shauri baya la dhuluma na kusema,
“Tumebuni mpango mkamilifu!”
Hakika nia na moyo wa mwanadamu vina hila.

Copyright information for SwhKC